Thursday 25 February 2016

MHANDISI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA NA MKANDARASI WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA RUSHWA.




Taasisi ya kuzuia na kupamba na rushwa(Takukuru) imewafikisha mahakamani mhandisi wa halamshauri ya wilaya ya Geita na mkandarasi kwa  makosa ya rushwa.


Akisoma makosa hayo mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ,Mh.Ushindi Swalo mwendesha mashitaka wa takukuru Bw.Kelvin Marusuri ameieleza mahakama kuwa mnamo june 7/ 2009 na  September 21/2009 wakiwa  ofisi za halmashauri ya wilaya walitumia nyaraka kumdanganya mwajiri na kumsababishia hasara.

Watuhumiwa waliandaa nyaraka yenye maelezo ya uongo kuwa kazi imefanyika kwa kuzingatia makubaliano na hivyo mkandarasi anastahili kulipwa  pesa zote za mkataba licha ya kutambua kuwa kuna baadhi ya kazi za thamani ya tsh 10,326,200(milioni kumi laki tatu ishirini na sita elfu mia mbili) hazikufanyika kulingana na mkataba.

Walihofikishwa mahakamani ni mhandisi,Mathias Shoto akituhumiwa kwa kosa la kumdanganya mwajiri kinyume na kifungu cha 22 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 na kumsababishia mwajili hasara kinyume na kifungu cha 284a(1)cha kanuni ya adhabu sura 16 marejeo ya mwaka 2002.

Wengine ni Hamisi Allani Chande na mkandarasi ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya ujenzi ya Kidagaa,Bw.Peter Alexander.


Aidha mwandisi Mathias Shoto ameachiwahuru  kwa dhamana hadi kesi hiyo itakapotajwa tena ifikapo march 10/2016 huku watuhumiwa Hamis Chande na Peter Alexanda wakishindwa kukamilisha masharti ya dhamana na kwamba imeamuru warudishwe mahabusu.

No comments:

Post a Comment