Thursday 25 February 2016

STEVEN WASIRA AMKUNJA SHATI MPIGA PICHA BAADA YA KESI YAKE KUPINGA USHINDI WA ESTER BULAYA KUTUPILIWA MBALI NA MAHAKAMA.




              Wasira Akimfuata mpiga picha kwa lengo la kufuta picha alizopigwa.

Mwanasiasa mkongwe nchini, Steven Wasira jana alimvamia mpiga picha aliyekuwa akichukua picha zake wakati akitoka mahakamani, lakini akashindwa kutimiza azima yake ya kufuta picha.

Wasiran ambaye ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika wa Serikali ya Awamu ya Nne alifanya kitendo hicho akitoka kwenye jengo la Mahakama ya Biashara ambako maombi yake ya kukata rufaa ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa ubunge, jimbo la Bunda yalitupiliwa mbali  na Mahakama Kuu.

Katika kinyang’anyiro hicho cha ubunge, Wasira  ambaye amekuwa mbunge wa Mwibara tangu mwaka 1970 na baadaye mbunge wa Bunda hadi mwaka 2015, aliangushwa na Ester Bulaya wa Chadema katika uchaguzi wa Oktoba 25 mwaka jana. Waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari akiwamo walishuhudia tukio hilo.

 “Baadaye alitaka kumgonga kwa gari lake wakati akiondoka lakini ikashindikana.”
Akisimulia tukio hilo, Jamson alisema Wasira, ambaye amefanya kazi na serikali za awamu zote tangu katikati ya miaka ya 70, alichukizwa na kitendo chake cha kumpiga picha.

“Njoo, njoo hapa wewe kijana. Nakuambia futa hizo picha kwa usalama wako.Hivi mnatafuta nini maana mnanifuatilia tangu nikiwa kule Mahakama Kuu hadi huku Mahakama ya biashara,” alisema Wasira

Jitihada za Wasira kumnasa Jamson ziliendelea hadi nje ya eneo la mahakama ambako alimfuata kwa kutumia gari aina ya Toyota Land Cruiser (namba tunazihifadhi).

Katika kumfuatilia, gari la Wasira nusura limgonge mpigapicha huyo, lakini waandishi wenzake walimnusuru kwa kumsukumia pembezoni mwa barabara.

Juhudi za kumpata Wasira kuzungumzia sababu za kutaka kumshambulia mpiga picha huyo kwa kuchukua picha za tukio hilo, hazikuzaa matunda.

No comments:

Post a Comment