Friday 24 March 2017

WATU 522 WAMEATHIRIKA NA UGONJWA WA KIFUA KIKUU (TB) MWAKA JANA WILAYANI GEITA

Mganga Mkuu wa Mgodi wa dhahabu wa Geita(GGM) Kiva Mvungi,akizungumza na waandishi wa habari juu ya ushiri wa mgodi katika kutokomeza ugojwa huo. 


Mganga Mkuu wa Mgodi wa dhahabu wa Geita(GGM) Kiva Mvungi Akikabidhi t-shert kama zawadi kwa mwananchi.

Mratibu wa huduma za kifua kikuu na ukoma Halmashauri ya Wilaya Kizingi Madeni akitoa takwimbu ya ugonjwa wa TB.




Ikiwa leo  ni siku ya kifua kikuu duniani imebainika kuwa wagonjwa 522 Wilayani Geita  wamegundulika kuwa na  vimelea vya kifua kikuu
Akizungumza na waandishi wa habari ,Mratibu wa huduma za kifua kikuu na ukoma Kizingi Madeni,alisema  tatizo la kifua kikuu ni kubwa sana katika halmashauri ya wilaya hiyo.

“Tatizo la Kifua kikuu kwa wilaya yetu ni kubwa ambapo ukiangalia takwimu za mwaka jana  watu 522 wamegundulika kuwa na maambukizi ya kifua kikuu na  tangu January hadi February   watu 105 wameathirika na tatizo hili ukiangalia takwimu hii unaona idadi ni kubwa sana kwa hiyo bado inaitajika nguvu kubwa ikiwa ya kutoa elimu ya kifua kikuu”alisema Madeni.

Miongoni mwa maeneo ambayo yanaongoza kwa maambukizi ni pamoja na kwenye migodi ya uchimbaji madini maduka online  ilizungumza na  Mganga Mkuu wa Mgodi wa dhahabu wa Geita(GGM) Kiva Mvungi ambapo  wao kama mgodi wamekuwa wakishiriki kutokomeza kifua kikuu kwa kuchangia kwenye hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwa kutoa vifaa vya matibabu na kukarabati hodi za wagonjwa ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa wananchi na wafanyakazi.

“Kwasababu ya watu wanaotuzungukuka kuakikisha kwamba wanajikinga na kifua na wanatibiwa pasipo matatizo tumekarabati hospitali ya Mkoa ikiwa ni pamoja na kutoa vifaa vya matibabu lakini pa tumeendelea kutoa elimu kwa kushirikiana na halmashauri zote mbili”alisema Mvungi

Elibariki Mussa ni moja kati ya wananchi  Mkoani Geita ameshauli elimu kuendelea kutolewa zaidi kwani bado tatizo lililopo ni wananchi wengi hususani ni maeneo ya machimbo awana elimu juu ya maambukizi ya kifua kikuu.

Siku ya kifua kikuu duniani huadhimishwa Tarehe 24 Mwezi March kila mwaka ambapo kwa mwaka huu Kauli mbiu ni“Tuungane kutokomeza kifua kikuu”



No comments:

Post a Comment