Thursday 16 March 2017

MAREHEMU SIR. GEORGE KAHAMA AAGWA NA KUZIKWA JIJINI DAR ES SALAAM



Waziri  wa Habari Utamaduni  Sanaa  na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akitoa salamu za  pole  kutoka Serikalini katika tukio la kuaga mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali  ya Tanzania  katika nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George Clement  Kahama aliyefariki  tarehe  12 Machi 2017 katika Hospitali  ya Taifa Muhimbili tukio hilo limefanyika leo katika Ukumbi wa Mwalimu Julius  Nyerere  Dar es Salaam.


Katibu  Mkuu wa  Chama  cha Mapinduzi Bw.Abdurahaman Kinana akitoa salamu za rambirambi  za  Chama  wakati wa kuaga  mwili wa aliyekuwa  kiongozi wa Serikali ya Tanzania na Chama Cha Mapinduzi katika nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George  Clement  


Jaji Mstaafu Mhe.Joseph Sinde Warioba akitoa  salamu za pole wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali ya Tanzania  katika nyadhifa mbalimbali Marehemu  Sir. George  Clement  Kahama

 

Rais wa awamu  ya pili ya  Serikali ya Jamhuri  ya  Muungano wa Tanzania Mhe. Alhaji  Ally Hassan  Mwinyi akitoa  salamu  za  pole  katika  tukio la kuaga mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali  ya Tanzania  katika  nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George Clement Kahama


Waziri  wa Habari, Utamaduni, Sanaa  na  Michezo  Mhe. Nape Moses Nnauye akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali  ya Tanzania  katika nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George Clement Kahama

 

Rais wa awamu ya pili ya Serikali ya Jamhuri ya Muunganowa Tanzania Mhe. Alhaji Ally Hassan MwinyiakitoaheshimazamwishokwamwiliwaaliyekuwakiongoziwaSerikali ya Tanzania  katika nyadhifa mbalimbali Marehemu Sir. George Clement Kahama aliyefariki tarehe 12 Machi 2017 katika Hospitali  ya Taifa Muhimbili


Makamu  wa  Rais mstaafu katika Serikali  ya  awamu  ya  Nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Mohammed  Gharib  Bilal akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa kiongozi wa Serikali ya Tanzania  katika nyadhifa mbalimbali Marehemu  Sir. George  Clement  Kahama aliyefariki tarehe 12 Machi 2017 katika Hospitali ya Taifa  Muhimbili

 

Mjane wa Marehemu  Sir. George Clement Kahama Mama Janet Kahama (wa pili kushoto)  akiwa na familia yake wakati wa Tukio  la kumuaga  mume wake ambaye aliwahi kuwa kiongozi wa Serikali  ya Tanzania  katika nyadhifa mbalimbali aliyefariki tarehe 12 Machi 2017 katika Hospitali  ya  Taifa
Serikali imesema itaendelea kuenzi na kuheshimu mchango mkubwa katika kupigania maendeleo na ustawi wa jamii uliofanywa na marehemu  Sir George Kahama enzi za uhai wake alipokuwa kiongozi katika nyadhifa mbalimbali ndani na nje ya Tanzania.

Hayo yamesemwa leo Jijini  Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape  Moses  Nnauye alipokuwa akitoa salamu za Serikali katika tukio la kumuaga mmoja wa waasisi wa Taifa na Waziri msataafu marehemu  Sir Gorge Kahama aliyefariki dunia Machi 12 mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Waziri  Nape amesema kuwa  Sir  George Kahama alikuwa kiongozi mahiri na aliyetekeleza majukumu yake kwa ufasaha ambapo alikuwa miongoni mwa viongozi walioanzisha harakati za Serikali za uendelezaji wa mji wa  Dodoma ikiwa ni sehemu ya  kuimarisha makao makuu ya nchi.

Kwa  upande  wake  Katibu Mkuu wa  Chama  cha  Mapinduzi (CCM) Bw. Abdurahaman Kinana amemueleza  Sir George  Kahama kama kiongozi mahiri katika Chama aliyependa maendeleo kwa wananchi na Taifa kwa ujumla katika weledi wa hali ya juu na alikuwa mchapakazi.

Marehemu  Sir  George  Kahama amekuwa  Waziri  na Kiongozi kabla na Baada  ya Uhuru wa Tanzania  Bara  kuanzia awamu ya  kwanza  hadi  ya tatu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo amezikwa  leoJijini Dar es Salaam na ameacha  Mjane na  Watoto.

No comments:

Post a Comment