Friday 24 March 2017

NYUMBA 40 ZIMEEZULIWA MAPAA KUFUATIA MVUA KUBWA ILIYO NYESHA WILAYANI GEITA

Moja kati ya wananchi ambaye nyumba yake imebomolewa na mvua.
Nyumba iliyoangukiwa na Mti baada ya mvua kubwa kunyesha.
Baadhi ya wananchi wakiwa na Diwani wa Kata Buhala hala ,Mussa Kabesse katika aliyevaa Kofia.


Jumla ya Nyumba  40 kwenye kata ya Buhala hala Wilayani Geita zimeezuliwa na zingine kubomoka kutokana na mvua iliyonyesha usiku wa kuamkia juzi hali ambayo imesababisha baadhi ya wananchi kukoswa makazi.

Dafroza Kadike ni moja kati ya wananchi wa mtaa wa Mwatulole ameelezea kuwa siku hiyo majira ya saa moja usiku mvua kubwa ikiambatana na radi ilinyesha na kusababisha nyumba nyingi kuezuliwa na zingine kuanguka kutokana na upepo .

Aidha kwa upande wake John Slvesta,ameiomba serikali katika wilaya ya Geita kutoa msaada kwa watu ambao wameathirika kwani wananchi wengi kwasasa wapo nje kutokana na makazi yao kuharibiwa.

Diwani wa kata hiyo,Mussa Kabese amekiri kuwepo kwa hali hiyo na kwamba amewataka wananchi kuwa na subira kwani hataakikisha anafikisha kwenye kamati ya maafa iliyopo Mkoani Geita.

“Mimi Nikiwa kama kiongozi wa kata hii ya Buhala hala nimesikitishwa na kile ambacho kimetokea kwa wananchi kuharibiwa makazi yao kutokana na mvua iliyo nyesha niwaombe tu wananchi ambao wamepatwa na maafa haya kujiandikisha kwa watendaji”alisema Kabese.



No comments:

Post a Comment