Monday 20 March 2017

DC DODOMA AKUTANA NA KAMATI NDOGO YA MKOA YA URATIBU UJENZI WA UWANJA WA MICHEZO WA KIMATAIFA DODOMA



Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Christina Mdeme akizungumza na Kamati ndogo ya Mkoa inayoratibu Ujenzi wa mradi wa Uwanja wa Michezo wa Kimataifa utakojengwa katika kata ya Nala Mjini Dodoma


Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Mkoa ya Uratibu Mradi wa ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Kimatafa Bw.Salum Mkuya akitoa mrejesho wa mambo yaliyofanywa na Kamati yake kwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Christina Mdeme (Hayupo Pichani)   katika kuhakikisha Mradi huo unafanikiwa.


Mjumbe wa Kamati hiyo ambaye ni Mwanasheria kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Evordy Kyando akifafanua jambo kwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Christina Mdeme (Hayupo Pichani)  wakati Kamati hiyo ilipokutana na Mkuu huyo wa Wilaya. 



Mjumbe wa Kamati hiyo ambaye ni Afisa Tawala Wilaya ya Dodoma Bw. Hashimu Kitambuliyo akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Christina Mdeme (Hayupo Pichani) kuhusu mipango na mikakati iliyoweka na Kamati hiyo katika kufanikisha Mradi huo.

No comments:

Post a Comment