Monday 27 March 2017

MTU MMOJA AFARIKI DUNIA KWA KULIWA NA MAMBA MKOANI GEITA



Mtu mmoja wilayani chato mkoani geita amefariki dunia baada ya kuliwa na mamba wakati alipo kuwa katika  shughuli zake za uvuvi wa samaki  katika ziwa victoria.
Tukio hilo limetokea  katika kijiji cha rubambangwe  wilayani chato  ambapo mtu huyo alikuwa katika shughuli zake za kila siku za uvuvi wa samaki  ndipo alipo vamiwa na mamba  kisha kumjeruhi vibaya katika sehemu zake za mwili nakupelekea  umauti.

Akizungumza mwenyekiti wa kijiji hicho Bw. Pasikali Maliyatabu amesema kuwa kumekuwa na matukio ya mara kwa mara ya watu  wanao  jishughulisha katika masula ya uvuvi wa samaki katika ziwa hilo kukamatwa  na kuliwa na mamba kwani tukio hilo nila tatu kutokea  katika kijiji hicho ambapo siku za nyuma watu wawili warifariki dunia kwa kuliwa na mamba .

Aidha mwenyekiti  huyo amemtaja aliyefariki dunia kuwa ni Emmanuel John mwenye umri wa  miaka 52  mkazi wa kijiji cha Rubambangwe wilayani chato.


Kwa upande wa baadhi ya wananchi wa kijiji hicho  Bw. Alex  Nagabona  na  Bi. Meresiana Bagaile wameiomba serikali kupitia halmashauri ya wilaya ya chato kufanya utaratibu wa kuwaondoa wanyama wakali wanaoishi kandokando ya ziwa hilo  kwani wamekuwa tishio jambo ambalo linawafanya kushindwa kufanya shughuli za uvuvi  huku wakihofia mamba pamoja viboko ambao wamekuwa  wakijitokeza  mara kwa mara na kuleta madhara kwa wavuvi.

No comments:

Post a Comment