Wednesday 1 March 2017

WANANCHI KUTOLIPWA FIDIA ZOEZI LA NGUZO LITAKAPO ANZA KUTEKELEZWA



Mkuu wa wilaya ya Geita, Mwl. Herman Kapufi.
Serikali wilayani na mkoani geita imesema haita walipa fidia wananchi watakao bomolewa nyumba zao au kukatiwa miti  pindi zoezi la usambazaji wa nguzo za umeme vijijini  litakapo kuwa limeanza  kutekelezwa. 

Hatua hiyo imekuja baada ya kuwepo kwa maeneo mengi  wilayani geita ambayo hayajapatiwa umeme kutokana na miundo mbinu kuwa duni ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba za makazi  kiholela jambo ambalo limesababisha shirika la umeme tanzania (TANESCO)kushindwa kupitisha nguzo kwasababu  hiyo.

Akizungumza na wananchi katika mamlaka ya mji mdogo  wa katoro mkuu wa wilaya ya Geita Hermani Kapufi amesema kuwa serikali itapeleka nguzo maeneo ambayo hayajapatiwa umeme kutokana na hilo hakuna mwananchi atakae lipwa fidia kama nyumba au miti yake itakuwa kandokando ya ramani ambapo nguzo za umeme zinatarajia kupita katika maeneo hayo.

Aidha kapufi amewataka wananchi walio tandaza nyaya katika nyumba zao wategemee kufungiwa umeme mwezi wa tatu na wanne na kwa wale ambao hawaja tandaza nyaya katika nyumba zao waweke ili zoezi hilo lifanyike kwa pamoja.






No comments:

Post a Comment