Thursday 9 March 2017

PLAN INTERNATIONAL YAKABIDHI KITUO CHA MALEZI AMBACHO KIMEGHARIMU 34,403,490 MKOANI GEITA.

Meneja wa Plan Intarnational Mkoani Geita Gratian Mushema Kweyamba  na Mgeni Rasimi ambaye ni afisa ustawi wa jamii wilaya ya Geita Anderson Shimbi wakizindua kituo cha malezi ya awali kwa watoto kwenye kijiji cha Magenge.

Jiwe la msingi likiwa katika kituo cha malezi

Darasa la watoto kwaajili ya kujifunza mambo mbali mbali ambayo ni msingi wa maisha yao.

Bango linaloelekeza kituo kilipo.

Wananchi wakishuhudia tukio la uzinduzi wa kituo hicho.

Afisa mtedaji wa kata ya Magenge Julius Fumbuka akitoa utambulisho wakati wa hafra fupi ya uzinduzi wa kituo.

Meza kuu 


Wananchi wakisikiliza kwa makini.

Meneja wa Plan Intarnational Mkoani Geita Gratian Mushema Kweyamba akielezea malengo ya mradi huo.

Msimamizi wa mradi huo Lydia  Wanjala akitoa maelezo ya namna zoezi la mradio huo lilivyofanyika.

Afisa mtendaji wa Kijiji cha Kaseme,Ndakilwa Ng'wanzalima akielezea namna ambavyo kituo hicho kitakavyoleta faida kwa wananchi na watoto katika kata hiyo.

Ukumbi wa mikutano kwaajili ya watoto.

Vifaa vya michezo mbali mbali.

Diwani wa kata ya Kaseme Andrea Kalamla ,akiomba ujenzi wa kituo hicho kujengwa pia kwenye kata yake.

Diwani wa kata ya Magenge,Edward Misungwi akihaidi kusimamia vikali kituo hicho.

Mgeni Rasimi ambaye ni afisa ustawi wa jamii wilaya ya Geita Anderson Shimbi,akisisitiza utunzaji wa vifaa vilivyopo kwenye kituo hicho.

Choo cha watoto.

vyoo vya walimu.

Picha ya pamoja .


Shirika lisilo la kiserikali la Plan International Mkoani Geita limekabidhi kituo cha malezi na makuzi ya awali kwa watoto wadogo chenye thamani ya sh,milioni thelathini na nne laki nne na  elfu tatu mia nne na tisini katika kata na kijiji cha Magenge wilayani hapa.

Akizungumza katika makabidhiano hayo na serikali ya kijiji,yaliyofanyika leo meneja wa Plan Mkoani humo Gratian Mushema Kweyamba,alisema kuwa lengo la ujenzi wa kituo hicho ni kumsaidia mtoto ambaye  yupo  chini ya umri wa miaka sifuri  hadi miaka mitano  (5) ambapo anaweza kujifunza mambo mbali mbali ya msingi.

“Tunaamini kuwa kituo hiki kitawasaidia watoto kupata elimu ya kujitambua wakiwa bado wadogo na ndio maana kauli mbiu yetu tunasema plan watoto kwanza,  tunaamini kuwa mtoto akijengewa misingi mizuri pamoja na malenzi yaliyomema  anaweza kuwa msaada kwa serikali na jamii inayomzunguka”Alisema Kweyamba.

Akielezea mafanikio ya ujenzi wa mradi huo,msimamizi wa kituo Bi,Lydia Wanjala,amefafanua  kuwa  tangua waanze ujenzi wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na jamii ambayo ipo eneo husika  kutoa ushirikiano kwa kiasi kikubwa .

Akimwakilisha Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ,Afisa ustawi wa jamii ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi kwenye makabidhiano hayo Anderson  Shimbi  aliwashauri wanakijiji kuwa waangalizi wa mradi huo na kuutunza kwa uangalizi mkubwa zaidi.

“Ndugu zangu wanakijiji gharama iliyotolewa hapa ni kubwa sana hivyo tunatakiwa sisi wenyewe  tuwe watu wa kwanza katika utunzaji wa mali hizi zilizopo kwenye kituo hiki”alisema Shimbi.

Diwani wa kata ya Magenge,Edward Misungwi,ametoa ahadi ya kuhakikisha wanakuwa walinzi wakubwa wa mradi huo na kwamba kwa mwananchi ambaye  ataonekana kukiuka masharti yaliyowekwa hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE.


No comments:

Post a Comment