Monday 6 March 2017

WAKAZI WA KATORO MKOANI GEITA WAMEIOMBA SERIKALI KUZUIA UUZAJI WA SILAHA ZA JADI KIHOLELA



Wananchi katika mamlaka ya mji mdogo wa Katoro wilayani na mkoani  Geita wameiomba Serikali kupiga marufuku uuzaji wa silaha za jadi kiholela ili kuepuka madhara yanayo weza kujitokeza katika jamii kutokana na silaha hizo kuuzwa pasipo kufuata utaratibu.
Wakizungumza  baadhi ya wananchi hao wamesema kuwa kumekuwepo na idadi kubwa ya watu katika eneo hilo ambao wanajishughulisha na  biashara hiyo ya uzaji wa silaha za jadi kiholela jambo ambalo linahatarisha usalama wa watu kutokana na silaha  hizo kufikia hatua ya kupangwa kandokando ya barabara  na kwenye mirundikano mikubwa ya watu  ikiwa ni pamoja na kwenye viwanja vya michezo.

Aidha wamezitaja silaha  zinazo uzwa katika maeneo hayo ni pamoja na mikuki , mishale, visu,shoka, sime pamoja na mapanga.

Kwa upande wao wafanya biashara wa silaha hizo Bw. Masalu Rukasi na Gervas Manyilizu wameeleza kuwa kabla ya kuingiza sokoni zana hizo kwa ajiri ya biashara  wanakuwa na kibali kutoka kwa kiongozi wa eneo husika kwa sababu ya usalama zaidi.

Wafanyabiashara hao wamesema  kumekuwepo na baadhi ya watu wanao kiuka taratibu hizo  ambazo wanatakiwa kufuata na badala yake  huuza zana hizo kihole kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa raia katika jamii.


aidha mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo wa katoro  Japheti Madoshi amewataka wanao jishughulisha na biashara hiyo kandokando ya barabara na kwenye mirundikano mikubwa ya watu waache mara moja  na badala yake watafute sehemu iliyo salama kwa ajiri ya biashara hiyo ikiwa ni pamoja na kujenga vibanda vya kuhifadhia zana hizo.

No comments:

Post a Comment