Wananchi
wa Kijiji cha Nandagwa Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi wakimlaki Mke wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli aliwapowasili eneo hilo
kwa ajili ya kutoa Msaada wa Vyakula, Mafuta pamoja na Dawa kwa ajili ya Kambi
ya Wazee ya Nandanga iliyopo katika kijiji hicho.
Mratibu
wa kambi ya Kulea wazee na watu wenye ulemavu ya Nandanga Bw. Agnerus Chiamba
akimpa maelezo Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth
Magufuli kuhusu nyumba za malazi katika kambi hiyo, aliwapowasili eneo hilo kwa
ajili ya kutoa Msaada wa Vyakula, Mafuta pamoja na Dawa.
Baadhi
ya Vitu vilivyotolewa kwa ajili msaada katika kambi ya kulea Wazee na watu
wenye ulemavu ya Nandanga.
Mkuu
wa Mkoa wa Lindi Mh. Godfrey Zambi akimkabidhi Mke wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli taarifa ya utekelezaji wa miradi
mbalimbali ya Maendeleo.
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli
akiongea na wananchi wa Kijiji cha Nandanga kilichopo Wilayani Ruangwa Mkoani
Lindi na kuahidi kuendelea kusaidia kambi hizo za wazee na watu wenye ulemavu
wa ukoma ambapo mpaka sasa meshatoa msaada katika kambi 4 katika mikoa ya Dar
es Salaam, Mwanza, Lindi na Mtwara yenye thamani ya Takribani shilingi 250.
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akiagana na
wananchi wa Kijiji cha Nandanga kilichopo Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi baada
ya kutoa msaada katika kambi ya kulea wazee ya Nandanga iliyopo eneo hilo.
No comments:
Post a Comment