Thursday 25 January 2018

SHIRIKA LA JSI LAENDELEA KUTOA MSAADA WA KUPAMBANA NA WATOTO WAISHIO KWENYE MAZINGIRA MAGUMU GEITA


DSC_1245
Mkurugenzi wa JSI kanda ya ziwa Dr Amos Haki Nsheha akimkabidhi Baiskeli Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Geita,Elisha Lupuga kwaajili ya kuwapatiwa  wasimamizi wanaotoa huduma kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi.

DSC_1210
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Geita,Elisha Lupuga akijaribia kuendesha baiskeli ambayo imetolewa na shirika lisilo la kiserikali la JSI.
DSC_1241
Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita,Ali Kidwaka akikabidhiwa Baiskeli na Mkurugenzi wa JSI kanda ya ziwa Dr Amos Haki Nsheha 

DSC_1221
Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita,Ali Kidwaka  Akisoma taarifa ya shukurani kwa shirika hilo.

Na,Joel Maduka,Geita

Shirikia lisilo la kiserikali la JSI limetoa Baiskeli 32 na makabati 13 kwa ajili ya kuendeleza mapambano dhidi ya unyanyasaji wa watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi .

Akizungumza baada ya kugawa Baiskeli hizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mkurugenzi wa JSI kanda ya ziwa Dr Amos Haki Nsheha amesema wilaya hiyo ina watoto wengi wanaoishi katika mazingira hatarishi. 

Alisema watoto hao wanafikia karibu elfu 20 na kwamba kutokana na mazingira wanayoishi wana hatari ya kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi kutokana na kufanyiwa vitendo viovu ikiwemo kubakwa.

Afisa ustawi wa Jamii wa wilaya ya Geita Bw Anderson  Shimbi amesema matukio ya ukatili kwa mwaka jana yalikuwa 97 kutoka kata 37 ambapo wanaume ni 40 na wanawake 57 na kwamba ukatili unaofanywa zaidi ni vipigo, ubakaji na wengine kutopewa nafasi ya kwenda shule .

Mmoja kati ya wasimamizi wanaotoa huduma kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi, Bw Tom Jarusinga amesema msaada huo umetolewa katika wakati muafaka kwani wengi wao walikuwa na shida ya usafiri wa kuwafikia watoto wanaofanyiwa ukatili.

Mkurugenzi wa Halmashauri wa wilaya ya Geita Bw Ali Kidwaka amesema mchango huo utasaidia kuelekea kwenye malengo ya dunia ya kupambana na ukimwi na kufikia malengo ya asilimia 90 ya watu wote wenye maambukizi kujua hali zao.

No comments:

Post a Comment