Tuesday 14 June 2016

WIZARA YA AFYA NCHINI KUENDESHA ZOEZI LA UPULIZAJI WA DAWA YA UKOKO MAJUMBANI MKOANI GEITA



Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga.

Wizara ya Afya,maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la ABT ASSOCIATES  inategemea kuendesha zoezi la upuliziaji wa Dawa ya Ukoko majumbani katika halmashauri ya mji wa Geita, na zoezi hilo linategemea kuanza tarehe 15 juni mwaka huu

Akizindua zoezi hilo katika viwanja vya halmshauri ya Mji mkoani hapa, mkuu wa mkoa wa Geita, Meja Jenerali mstafu Ezekiel Elias kyunga, amesema kuwa malaria bado ni ugonjwa unaoongoza kwa vifo na  kwa Tanzania ni miongoni mwa nchi 10 za Afrika ambapo sehemu kubwa watu wake wapo katika hatari ya maambukizi ya Malaria, huku zaidi ya asilimia 93 ya wananchi wanaoishi  wapo kwenye maeneo yenye hatari ya maambukizi ya Malaria Nchini.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM), Bw.Isack Senya,amesema kuwa lengo la Mgodi kudhamini mradi huo ni kuhakikisha kuwa Wananchi wanaouzunguka Mgodi wanakuwa katika hali ya usalama na zaidi wanakuwa katika afya njema,na amewataka wananchi kulipokea zoezi hilo na kukubali kushirikiana na        Halmashauri kuhakikisha kuwa wanakuwa mstari wa mbele kutokomeza malaria katika kaya zao.

Aidha kwa upande wao wananchi wamesema kuwa wamelipokea zoezi hilo kwa mikono miwili lakini wameiomba Serikali kuhakikisha kuwa inatoa Elimu ya kutosha kwa wananchi ambao wapo pembezoni mwa Mji ili kuweza kujinusuru na Janga la Maralia katika maeneo yaliyopo nje.


Takwimu za Dunia zinaonyesha kwamba wastani wa mtu mmoja anapoteza maisha kwa kila dakika moja inayopita kutokana na ugonjwa huu, pia ripoti ya dunia ya shirika la afya duniani ya mwaka 2012 ambapo malaria iliua takribani watoto laki 4 na elfu 82,000 wenye umri chini ya miaka mitano, Kitaifa inakadiriwa kuwa wastani wa wagonjwa wapatao elfu 60  hadi 80 hupoteza maisha kutokana na Ugonjwa wa Malaria kwa mwaka.

No comments:

Post a Comment