Wednesday 1 June 2016

BEI ZA MAFUTA YA PETROL, DIESEL NA MAFUTA YA TAA ZAANZA KUTUMIKA LEO

June 1, 2016 Mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji nchini (EWURA) imetoa bei mpya za mafuta ya taa na mafuta ya Petrol, Diesel katika masoko yote ya jumla na rejareja zimeanza kutumika leo.
Mkoa ambao unaonekana kuwa na bei nafuu kati ya hizi ni Tanga mjini ambapo bei ya kikomo ni Sh.1795/= kwa petrol huku bei ya juu Sh.1802/= katika wilaya ya Pangani, Mkoa mwingine ambao unaonekana kuwa na bei ya juu zaidi ni Kigoma ambapo kama ilivyokuwa mikoa mingine ya mipaka Lita moja ya petrol inauzwa kwa zaidi ya sh.2000/= huku wilaya ya Uvinza ikiwa zaidi ya Sh.2108/=.

No comments:

Post a Comment