Wednesday 22 June 2016

WATUMISHI WA SERIKALI WILAYANI BUKOMBE MKOANI GEITA WAASWA KUFANYA KAZI KWA UELEDI ZAIDI


Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga( katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe James Ihunyo

Watumishi wa Serikali Wilayani Bukombe mkoani Geita wametakiwa kufanya kazi kwa bidii na waledi ili kuleta maendeleo katika halmshauri hiyo.
Hayo yamesemwa na Afisa tawala Mkoani hapa, Selestine Gasimba katika Baraza maalumu la kujibu hoja za  CAG amesema kuwa nyakati zimebadilika hivyo ni vyema kujua kuwa wakati wa kufanya mambo kimzaa wakati huo umekwisha ni vyema kwa watendaji wakaongeza faida ya kufanya kazi kwa bidii zaidi.

Mkuu wa wilaya hiyo, Amani Mwenegoha amesema kuwa Halmashauri ambayo inatakiwa kujibu hoja za CAG ni halmashauri ambayo haijasimamia vizuri watendaji wake.


Diwani wa kata ya Uyovu, Yusuf Fungameza na Diwani wa Viti maalum Elizabeth Ngasa wamewalalamikia  wataalamu kufanya kazi kwa mazoea na kusababisha halmashauri yao kupoteza mali na mapato sanjari na hilo la kupewa na CAG hati ya mashaka.

No comments:

Post a Comment