Wednesday 22 June 2016

BAADHI YA WANANCHI MKOANI GEITA BADO HAWANA UELEWA JUU YA FAIDA ZA MATUMIZI YA UZAZI WA MPANGO


Baadhi ya wananchi Mkoani Geita bado hawaona kuwa uzaaji watoto wengi kuna athari kwa maendeleo ya nchi na kiafya kwa ujumla huku baadhi yao wakidai kuwa wamehalalishwa kuzaa hadi kizazi kitakapoisha.
Matumizi ya uzazi wa mapango hasa vijijini bado ni changamoto huku baadhi ya kaya zenye watoto wengi wanashindwa kuwapa mahitaji kama ya chakula,mavazi pamoja na huduma zingine kutokana na kuwa na watoto wengi huku wazalishaji katika familia ni wachache.
Baadhi ya wakazi mkoani hapa wanaona kuzaa ni tunu bila kujali athari za kiafya na kiuchumi na matatizo ya uzazi wa mpango mkoani geita hadi sasa ni asilimia 26 tu, na changamoto zimekuwa zikiwakumba baadhi ya wanawake wanapotaka kutumia njia hizo za uzazi wa mpango huku maeneo ya mjini kidogo kuna uelewa kwa jamii tofauti na kijijini
Utafiti uliofanyika hivi karibuni unaonyesha kuwa utumiaji sahihi  wa njia za uzazi wa mpango unasaidia kupunguza vifo kwa wajawazito kwa asilimia 40, msikilize mganga mkuu wa wilaya ya chato Alhamis Nyamagubi akielezea kuhusu hili

Takwimu za mkoa zinaonyesha waliopata ushauri wa huduma ya uzazi wa mpango ni wanawake kumi na nane elfu na arobain na tano, huku waliopata njia ya uzazi wa mpango baada ya kujifungua ni moja elfu mia sita thelathini na tano na waliopata uzazi wa mpango baada ya mimba kuharibika ni 165 na mwsho waliopata rufaa ya kwenda kliniki ya uzazi wa mpango ni moja elfu na mia tattu sitini na moja hata hivyo elimu bado inahitajika zaidi kwa jamii kuhusu Matumizi ya njia za uzazi wa mpango ili kuboresha hali ya familia na uchumi wa Taifa kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment