Friday 17 June 2016

WAZIRI NAPE AKUTANA NA WAKUU WA VITENGO VYA MAWASILIANO SERIKALINI KATIKA KUADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA



Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO Bi. Zamaradi Kawawa akisalimiana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye wakati akiwasili katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO ili kuzungumza na Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini Jana Jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye (katikati) akiongea na Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini (hawapo pichani) ambao aliwataka kutengeneza mikakati madhubuti itakayoimarisha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO Bi. Zamaradi Kawawa na kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Jamal Zubeir.






Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini Leo Jijini Dar es Salaam.




Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini wakimsikiliza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye wakati wa kikao cha pamoja ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya utumishi wa umma. 





Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Bi. Prisca Ulomi akitoa neno la shukrani kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye kwa niaba na Maafisa Mawasiliano wakati wa kikao cha pamoja kilichofanyika leo Jijini Dar es Salaam.





No comments:

Post a Comment