Thursday 9 June 2016

MKUU WA IDARA YA KILIMO NA MIFUGO HALMASHAURI YA WILAYA (DALDO) CHATO NA MAWAKALA WA PEMBEJEO ZA KILIMO WAHUKUMIWA KWA MAKOSA YA RUSHWA

Mkuu wa idara ya kilimo na mifugo halmashauri ya wilaya (DALDO) Chato na mawakala wa pembejeo za kilimo wamehukumiwa kwa makosa ya rushwa .
Mahakama ya wilaya ya Chato mkoani Geita imewatia hatiani na kuwahukumu washitakiwa 4 kwa makosa mbalimbali ya uhujumu uchumi, katika kesi 4 tofauti.

Waliotiwa hatiani na kuhukumiwa  kati ya washitakiwa wengine walioachiwa huru ni aliyekuwa mkuu wa idara ya kilimo na mifugo (DALDO) wilayani Chato dk. Fares Nyamsimbwa Tongora pamoja na waliokuwa mawakala wa pembejeo za kilimo wa wilaya hiyoo bw. Sephania Endelyasi Mahenge  na bi Mary David Mwamgogwa.

Washitakiwa walipatikana na hatia na kuhukumiwa tarehe 6/6/2016 mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Chato mh.Jovith Kato  na mwendesha mashitaka wa takukuru bw Kelvin Murusuri katika mashauri tofauti ya uhujumu uchumi ma 4 kati ya ma 5 yaliyotolewa uamuzi ambayo ni ecc 01/2015, ecc 01/2014, ecc 04/2013, na ecc 06/2013.

Washitakiwa walikuwa wanakabiliwa na makosa ya rushwa yaliyotokana na ugawaji wa pembejeo za kilimo kwa wananchi katika msimu wa kilimo wa mwaka 2010/2011.

Dk. Fares Nyamsimbwa Tongora alipatikana na hatia na kuhukumiwa jumla ya makosa 12 ya kula njama ili kutenda kosa, kusaidia kutenda kosa, na matumizi mabaya ya madaraka ya umma kinyume na vifungu namba 30, 31, na 32 sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007.mshitakiwa atahukumiwa kwenda jela  miaka 12 au kulipa faini jumla ya tsh. million 2 ,000,000/= . mshitakiwa alilipa faini .

Mh.Jovith Kato alieleza kwamba dk. Fares Nyamsimbwa Tongora alishindwa kutimiza majukumu yake kwa uzembe hivyo kusababisha serikali kushindwa kuwafikishia wakulima pembejeo za kilimo na serikali kuwalipa mawakala fedha ambazo hawaku kustahili.

Aidha wakala wa pembejeo bw.Sephania Mahenge alitiwa hatiani na mahakama kwa jumla ya makosa 40 katika kesi 2 ambazo ni namba ecc 01/2015 na namba ecc 06/2013 na kuachiwa huru katika kesi namba ecc 05/2013.

Naye  bi Mary David Mwamgogwa alikutwa na hatia katika makosa 40 katika kesi za uhujumu uchumi namba ecc 04/2013 na ecc 1/2014, ambapo mawakala wote wawili bw. Sephania Mahenge na bi Mary Mwamgogwa walitiwa hatiani kwa makosa ya  kughushi nyaraka kinyume na vifungu na 333,335 na 337 na kutengeneza nyaraka za uongo kinyume na kifungu cha 342 vyote  vya sheria ya kanuni ya adhabu( cap 16 ya mwaka 2002).

Mahakama ilimhukumu bw.Sephania Mahenge  kulipa faini jumla ya tsh.laki 900,000/= au kwenda jela jumla ya miaka 4 kwa makosa 40 ya kesi 2 alizopatikana na hatia. mshitakiwa alilipa faini.

Hata hivyo mahakama haikuweza kusoma adhabu dhidi ya bi Mary David Mwamgogwa kwa sababu ya kutokuwepo mahakamani na itasoma atakapopatikana.

Mkuu wa takukuru mkoa wa Geita bw. Thobias Ndaro ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa geita kuendelea kuiunga mkono takukuru na serikali kwa ujumla katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kutoa taarifa mbalimbali za vitendo vya rushwa na ubadhilifu katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na vitendo vinavyofanyika kwenye ofisi za serikali za mitaa, mahakama na halmashauri ili watuhumiwa waweze kuchukuliwa hatua za kisheria na hivyo kushiriki kutokomeza vitendo vya rushwa, ubadhilifu na ufisadi katika jamii zetu na hivyo mwananchi atakuwa ameshiriki kukata mnyororo wa rushwa.



No comments:

Post a Comment