Wednesday 29 June 2016

WADAU MBALIMBALI WA ELIMU MKOANI GEITA WAOMBWA KUCHANGIA SUALA LA KUBORESHA ELIMU


Wadau wa elimu Mkoani na wilayani Geita,wameombwa kujitokeza kuchangia suala la elimu, ikiwa ni pamoja na kutoa madawati kwaajili ya kutengeneza mazingira bora ya kupatia elimu kwa wanafunzi.

Rai hiyo imetolewa na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Geita, Ally Kidwaka,wakati alipokabidhiwa madawati 240 yenye thamani ya milioni 12 na laki 6 kutoka kwa mjasiliamali Evarist Gervas, na kusema kuwa  ni vyema kuhakikisha kuwa kila mdau anashiriki vyema katika kuchangia madawati ili kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza mara kwa mara kutokana na uhaba wa madawati.

Kwa upande mwingine Afisa elimu wilayani hapa, Deus  Seif  amesema kuwa upungufu wa madawati kwa wilaya ya Geita ni mkubwa  hali ambayo inawalazimu watoto wengi kusoma wakiwa wamekaa chini.

Aidha kwa upande wake Evarist Gervas, amewaomba  wafanyabiashara na wananchi wengine kwa ujumla kujitokeza kuunga juhudi za kusaidia elimu katika maeneo wanayoishi huku  akionesha mfano kwa kuwa mchangiaji mzuri katika masuala ya elimu tangu mwaka 2013 alipotoa madawati na kujenga madarasa.


Diwani wa Kata ya Nyarugusu, Swalehe Juma amemshukuru  mfanyabiashara huyo kwa kuonyesha moyo wa upendo kwa kujitolea kuchangia na kuunga mkono suala la elimu.

No comments:

Post a Comment