Monday 20 June 2016

EWURA YAKANUSHA TAARIFA ZA UHABA WA MAFUTA NCHINI

Leo June 20 2016 baadhi ya magazeti yameibuka na taarifa ambazo imedai kuwa mafuta ya taa yameadimika katika mikoa kadhaa nchini ikiwamo Dar es salaam, Morogoro, Mwanza, Mtwara na Mikoa ya Kanda ya Kaskazini.
Mkurugenzi wa mafuta ya  Petrol kutoka mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na Maji(EWURA) injinia Godwin Samweli amekanusha taarifa hizo na kusema hakuna upungufu wa mafuta ya taa nchini kwa sababu yapo ya kutosha na meli kubwa imemaliza kushusha lita milioni 2.5 ambazo zitatumika kwa siku 20 na mengine yapo kwenye matanki.
tuna mafuta mengi tu, mengine yameshuka leo na mengine yako kwenye matanki, kila mwezi lazima kuna shehena ya mafuta ya taa inakuja, kwa siku moja kwa matumizi yetu ni kama  lita 126,000‘

hakuna mfanyabiashara atakuwa na pampu ya mafuta ya taa halafu akatae kuuza mafuta ya taa, kama kuna mkoa mmoja au miwili ambayo imetokea hivyo huenda gari limeharibika njiani, lakini wafanyabiashara wako makini sana kufanya biashara, kama mafuta yapo hapa Dar es salaam ni lazima watayapeleka kwenye vituoa vyao

No comments:

Post a Comment