Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetangaza kiama kwa wafanyabiashara wa vifaa vya mawasiliano, kuacha kuwahadaa wananchi kwa kutoa punguzo ili kuwashawishi kununua simu bandia na kutishia kuwafunga miaka 10 jela, faini ya Sh30 milioni au vyote kwa pamoja watakaobainika.

Wanawake wawili akiwemo mhudumu wa afya wa zahanati ya Kagu iliyopo kijiji cha Kagu Elizabeth Misango [54] na wa pili Helena Paulo [56] mkazi wa kijiji cha Luhuha mkoani Geita wameuawa kwa kukatwa katwa kwa mapanga ikiwemo kuchinjwa shingoni katika matukio mawili na maeneo tofauti usiku wa April 21.