Friday 1 April 2016

WATU 11 WARIPOTIWA KUWA NA UGONJWA WA KIPINDUPINDU MKOANI GEITA


Watu kumi na moja wameripotiwa kuwa na ugonjwa wa Kipindupindu katika mji mdogo wa Katoro mkoani Geita ambao unasadikika  kuibuka kwa mara nyingine  kuanzia  jana machi 31baada ya watu wanne kugundulika kuwa na dalili za ugonjwa huo.

Akizungumza na Storm habari mganga mfawidhi wa kituo cha afya  Katoro bw Peter Janga , amesema  kuwa amepokea watu kumi na moja wanaodaiwa kuwa na ugonjwa wa kipindupindu na kwamba kwa sasa wanaendelea kufanyiwa matibabu katika kituo hicho.

Kwa upande wake mwenyekiti wa  mamlaka ya mji mdogo wa Katoro bw Japheti Madoshi  amekiri kuwepo kwa wagonjwa  wa kipindupindu katika kituo hicho na kwamba wameweka mikakati madhubuti ya kukabiliana na ugonjwa huo ambao umekuwa hatarishi katika maisha ya wananchi nchini.

Aidha mwenyekiti huyo amewataka wananchi wa mji huo kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na kusafisha mazingiza yao kuchemsha maji ya kunya na kuacha kutumia vyakula vya baridi hali ambayo itawasaidia kujikinga na maabukizi ya ugonjwa huo.

No comments:

Post a Comment