Monday 4 April 2016

WAFUGAJI WILAYANI BUKOMBE MKOANI GEITA WALALAMIKIA SUALA LA UNYANYASWAJI.


Wafugaji wilayani Bukombe Mkoani Geita  walalamika juu ya unyanyasaji na mateso wanayofanyiwa na askari wa pori la akiba la kigosi muyowosi kwa kwa kupigwa viboko,kutozwa faini zisizo na risiti na kutishiwa kupigwa risasi kutokana na kufuga mifugo yao katika pori hilo.

Wakizungumza mbele ya mawaziri wa maliasili na utalii Jumanne Maghembe na waziri wa kilimo mifugo na uvuvi Mwigulu Nchemba wamedai kuna wenzao wameshapoteza maisha na mifugo mingi kupigwa risasi na kuwaacha baadhi ya wafugaji katika wimbi la umasikini.
aidha wanakabiliwa na uhaba wa maeneo ya malisho na tayari yaliyotengwa yanatumiwa na wakulima na mengine ni makazi ya watu.baadhi ya wafugaji wanaelezea kuwa wamekuwa na kilio hiki kwa muda mrefu na kudai wameshafanyia vikao vingi na viongozi wa serikali lakini muafaka wa kudumu haujapatikana.
Hata hivyo baadhi ya viongozi wa Serikali wanadaiwa kuwa chanzo cha matatizo yanayotokea huku Mbuge wa Bukombe Dotto Biteko anadaiwa kutumiwa na wafugaji.

Katika pori la muyowosi kuna ng`ombe zaidi ya milioni mbili na serikali ipo katika mpango wa kutafuta maeneo,katika hatua nyingine wafugaji wamepewa muda kufikia june 15 wawe wameondoka katika pori hilo hata hivyo chama cha wafugaji kanda ya ziwa kimeomba kupata suluhu ya kudumu ili wafugaji wajikite katika kukuza uchumi wao na taifa kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment