Friday 23 September 2016

FAHAMU MECHI ATAKAZOZIKOSA LIONEL MESSI BAADA YA KUPATA JERAHA KATIKA MGUU WAKE(GROIN)


Usiku wa Septemba 21 Ligi Kuu Hispania iliendelea kama kawaida kwa michezo kadhaa kupigwa, lakini moja kati ya michezo iliyochezwa ni pamoja na mchezo kati ya FC Barcelona dhidi ya Atletico Madrid uliomalizika kwa sare ya goli 1-1.
FC Barcelona ambao walikuwa katika uwanja wao wa nyumbani walipata pigo katika mchezo huo ambapo mchezaji wao tegemeo Lionel Messi aliumia mguu wake wa kulia dakika ya 51 na kutolewa nje na nafasi yake kuchuliwa na Arda Turan.


Leo Septemba 22 2016 taarifa zimetoka Lionel Messi atakaa nje ya uwanja kwa wiki tatu na atakosa michezo sita dhidi ya Sporting Gijon, Gladbach, Celta Vigo, Deportivo la Coruna na anatazamiwa kuwa fiti katika mchezo wa UEFA Champions League dhidi yaMan City October 19 2016.

No comments:

Post a Comment