Tuesday 12 April 2016

MADEREVA MKOANI GEITA WASHAURIWA KUFUATA KANUNI ZA BARABARA ILI KUEPUSHA AJALI ZA MARA KWA MARA

Madereva  wa vyombo vya moto mkoani Geita wameshauriwa kuhakikisha wanafuata  kanuni na sheria za barabarani  ili kuepusha ajali ambazo zimekuwa zikitokea  mara kwa mara na kusababisha  vifo  vya watanzania   wengi.


Hayo  yamesemwa  na mwakilishi wa mkuu wa kitengo cha usalama barabarani (RTO) mkoani hapa,sajenti  Deus Mgema,wakati wa uzinduzi wa mafunzo  ya usalama barabarani  yanayotolewa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Greenmood Organization.

Amesema kuwa  ni vyema kwa dereva  anapokuwa barabarani kuwa na nidhamu pindi anapokuwa akiendesha chombo cha moto ikiwa ni pamoja na kufata kanuni za usalama.

Kwa upande wake,bw Falesi Lujoja,amesema kuwa ni vyema kwa wanafunzi ambao wamekuwa wakijitokeza kwenye mafunzo hayo kutilia  maanani  kile wanachofundishwa.

Aidha mkurugenzi wa taasisi hiyo,Daniel  Makungu,ameeleza dhumuni la kufungua taasisi hiyo ni kuhakikisha  kila  mtu anayetumia  barabara anarudi akiwa salama nyumbani na kudhibiti ajali za mara kwa mara.

No comments:

Post a Comment