Saturday 16 April 2016

ZIKIWA ZIMEBAKI SIKU CHACHE MABASI YA MWENDO KASI KUANZA KAZI NCHINI WAZIRI MKUU ATOA AGIZO KWA TAASISI HUSIKA


Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya mradi wa mabasi yaendayo kasi kuanza, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaagiza wakuu wa taasisi zinazohusika na utekelezaji wa mradi huo kuhakikisha wanatoa elimu kwa umma ili kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza.

 Waziri mkuu amesema "Katika kipindi hiki cha majaribio, ambacho madereva wameanza kutumia barabara za BRT, hakikisheni mnatoa elimu ya kutosha kwa wananchi kuhusu namna ya kuvuka barabara, kuzuia wenye bodaboda kutumia barabara hizo kuelezea na matumizi ya taa za barabarani kwa madereva wote,”

No comments:

Post a Comment