Friday 1 April 2016

MAMLAKA YA UDHIBITI WA HUDUMA ZA NISHATI NA MAJI(EWURA) YASHUSHA BEI YA UMEME NCHINI.



Mamlaka ya Usimamizi na udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA)imetangaza kushusha bei za umeme kuanzia leo kwa watumiaji wote wa viwango tofauti.

Kushuka huko kwa bei ya umeme ni kutokana na ombi la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)kutaka bei za umeme zipunguzwe sambamba na hilo gharama za huduma kwa baadhi ya wateja zimeondolewa. 

Bei mpya  kwa watumiaji wadogo ni sh.100 kwa uniti, watumiaji wa kati ni sh.292  toka  298  ya  zamani.Wafanyabiashara wadogo ni sh. 195 toka sh. 200  ya  hapo  awali.

Bei mpya  kwa wafanyabiashara wa kati ni sh.157 toka sh. 159. Wanaonunua kwa wingi (bulk) ni sh. 152  toka  sh. 156  ya  hapo awali.

No comments:

Post a Comment