Tuesday 19 April 2016

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ATOA UFAFANUZI KWA WANANCHI WAISHIO MGUSU MKOANI GEITA BUNGENI HII LEO



Wananchi waishio  mtaa wa Mgusu wilayani na mkoani Geita wametakiwa  kujua kuwa wanaishi   katika sehemu ya leseni ya utafiti wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita( GGM) na kwamba  eneo hilo bado mgodi haujaona sababu  ya kulichukua.

Akiuliza swali katika  kipindi cha maswali na majibu Mbunge wa viti maalum CHADEMA  mkoani hapa Upendo Peneza, ametaka kujua kuwa serikali inaweka msukumo gani kwa mgodi kuhakikisha kuwa inawalipa wananchi fidia ili waweze kuondoka katika maeneo hayo.

Akijibu swali la mbunge wa viti maalum,mkoani hapa  Naibu Waziri wa nishati na madini Dkt.Merdad Kalemani amesema kuwa kwa sasa hivi eneo hilo bado halijaanza kutumika na kwamba mgodi hauoni sababu ya kulichukua .


Katika hatua nyingine pia wananchi mkoani hapa wamekuwa na maoni tofauti juu ya bunge la bajeti ya mwaka 2016/17 lililoanza rasimi hii leo mkoani dodoma.

No comments:

Post a Comment