Tuesday 12 April 2016

BAADA YA KUMTENGUA ANNE KILANGO, RAISI MAGUFULI ASEMA AMETUMA WATU KUWAREKODI MAWAZIRI WANAOLALAMIKA ILI NAO AWATUMBUE MAJIPU


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. John Pombe  Magufuli amesema amewatuma watu kuwarekodi mawaziri ambao wamesikika wakilalamika 'chinichini' kukatwa kwa fedha za matumizi mengineyo ( OC- Other Charges )  katika bajeti ya serikali ya mwaka ujao wa fedha.


"Mawaziri wengine nasikia wanalalamika kweli,sasa nimetuma watu kuwarekodi kwa sababu mind set (fikra) zao bado hazijabadilika,wanafikiri watu bado tupo kwenye trend  hiyo hiyo,wasomi ni wengi,unaweza ukawateua leo na kesho ukawabadilisha, ili mradi twende kwenye trend ninayoitaka," alisema Magufuli.

Rais Magufuli  aliyasema hayo jana Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia hatua ya bunge kubana matumizi na kuwezesha kupatikana kwa kiasi cha shilingi bilioni 6 ambazo zitaelekezwa kwenye utengenezaji wa madawati.

“Chief Secretary(Katibu Mkuu Kiongozi ), huo ndio muelekeo kwa Makatibu Wakuu, waache kudai OC… Nawasikia watu wanadai eti OC ni kidogo. Wakiona hazitoshi basi waache kazi, maana wenzao wabunge wamesema ni nyingi na wamebana matumizi," alisema Rais Magufuli na kuongeza:

No comments:

Post a Comment