Thursday 21 April 2016

MAKAMPUNI YANAYOZALISHA BIDHAA NCHINI YATAKIWA KUWEKEA NEMBO BIDHAA ZAO


Serikali kupitia wizara ya viwanda,Biashara na uwekezaji imeyataka makampuni yanayozalisha bidhaa nchini kusajili nembo za bidhaa zao ili kuweza kupata takwimu sahihi ya bidhaa  zizalishwazo  Nchini.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda,Biashara na uwekezaji, Mkurugenzi wa uhamasishaji masoko katika Wizara hiyo Bw.Odilo Majengo amesema hatua hiyo itapanua zaidi soko na kuitangaza Tanzania kwa uzalishaji wa bidhaa kwa mataifa mengine.

Yote hayo yalizungumzwa katika hafla ya kusaini makubaliano ya ushirikiano kati ya shirika la viwango Tanzania TBS na kampuni ya GSI Tanzania Ltd yenye jukumu la kusimamia alama za utambuzi wa bidhaa.


Katika hatua nyingine pia kampuni ya GSI Tanzania Ltd ambayo pia inahudumia nchi jirani za Rwanda,Burundi,Uganda,Zambia na Malawi ilikabidhi vyeti kwa wazalishaji 14 walioojiunga na huduma za kampuni hiyo kwa robo ya kwanza ya mwaka 2016

No comments:

Post a Comment