Thursday 28 April 2016

HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA KUBORESHA VITUO VYA AFYA

 
Halmashauri  ya wilaya ya Geita mkoani hapa imedhamiria  kuboresha vituo vya afya ili kuweza kutoa huduma zinazolingana na hospitali ya wilaya ili kupunguza idadi ya vifo vya akina mama wajawazito pamoja na watoto.

Yayo yamesemwa na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Geita bw,Ally Kidwaka katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Musanyenge ndani ya mji wa Katoro ambapo ameeleza kuwa kutokana na kuwepo kwa ongezeko kubwa  la idadi ya watu katika mji huo inatakiwa kuwepo hospitali yenye hadhi ya wilaya.


Aidha Kidwaka ameongeza kuwa wameweka mipango madhubuti ya kuboresha vituo vya afya ambapo wataanza na vituo 2 wilayani hapa  ikiwemo kituo cha afya Katoro pamoja na kituo cha afya kilichopo Nzera.

No comments:

Post a Comment