Thursday 7 April 2016

UMOJA WA WAZAZI MKOANI GEITA WATOA TAMKO JUU YA JUHUDI ZA RAIS MAGUFULI



Umoja wa Wazazi Mkoani Geita umetoa tamko la kuunga mkono juhudi za dhati zinazofanywa na Rais Joseph Magufuli la kulikomboa Taifa la Tanzania litakaloweza kusimama na kujiongoza kwa kuwa na watendaji wanaoendana na kasi ya Rais.

Umoja huo umetoa tamko hilo wakati wa kuadhimisha kilele cha wazazi mkoani Geita na kuandaa ibada ya kumuombea raisi Maggufuli na nchi kwa ujumla.
Umoja huo umesema kwa muda mfupi usimamizi katika mapato ya serikali yamefanikiwa kwa kuziba mianya ya ukwepaji kodi na wana imani kubwa mapato ya taifa yatazidi kupanda na kuondokana na utegemezi.
Kutokana na uongozi mzuri wa awamu ya tano wanaamini mabadiliko yatazidi kuonekana na sifa za viongozi bora zitaonekana.

Katika hatua nyingine wamesema baadhi ya viongozi wa mataifa ya nje yamedaiwa hayawezi kumuunga mkono kiongozi wa Afrika anayefanya vizuri.

No comments:

Post a Comment