Wednesday 4 January 2017

MAAMUZI YA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA KUHUSU MAUAJI YA WAKULIMA NA WAFUGAJI



Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba alifika katika kijiji cha Tindiga kilichopo wilaya ya Mikumi zilipotokea vurugu zilizopelekea mkulima mmoja kuchomwa mkuki mdomoni na kutokea shingoni na kusikiliza kero zinazowasumbua wananchi wa Kilosa kabla ya kutoa maamuzi. 
Waziri Mwigulu amesema kuanzia sasa likitokea tukio lolote la watu kuuana kwa mapanga, mikuki, sime  na silaha zozote za jadi zinazotumiwa hasa na wakulima na wafugaji, serikali itafuta utaratibu wa kubeba silaha hizo na atakayebeba atakamatwa na kuchukuliwa hatua kama watuhumiwa wengine.
Kinginie alichoagiza Waziri Mwigulu ni wakuliam na wafugaji kwa pamoja kuwakamata watu wote watakaohusika na kuanzisha vurugu na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola kabla jeshi la polisi halijafanya maamuzi yake.

Kuanzia leo tunaanza kuhesabu pakitokea tukio lolote la vurugu na zikatumika silaha kuwadhuru wananchi, tutafuta utaratibu wa watu kutembea na silaha mitaani, na ukikutwa nayo unakamatwa kama ambavyo mtu mtu mwenye silaha ya moto na hajaiandikisha. Hatuwezi kuruhusu hii ikawa nchi ya watu wanakatanakatana tu”alisema Mwigulu

No comments:

Post a Comment