Wajumbe wa Halmashauri ya chama cha mapinduzi wilaya ya Geita wakiwa
kwenye kikao.
Katibu wa siasa na uenezi Wilaya ya Geita Bw Jonathan
Masele Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa kikao cha
wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama.
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi Wilaya ya Geita,Barnabas Mhoja Mapande
akielezea juu ya wananchi kuendelea kumuunga Mkono Rais.
Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho wakichangia Hoja mbali mbali.
Katibu wa chama cha Mapinduzi(CCM)Wilayani Geita, Julius Peter Akielezea
namna ambavyo watanzania watanatakiwa kuendelea kufanya kazi kwa Bidii ikiwa ni
pamoja na kulipenda Taifa.
Akizungumza kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama hicho, Katibu wa
siasa na uenezi Bw Jonathan Masele alisema hatua zinazoendelea
kuchukuliwa na Rais Magufuli zitasaidia maendeleo ya nchi na Taifa litanufaika
na Rasilimali zilizokuwa zikipelekwa nje ya nchi bila utaratibu.
“Tunatambua kuwa juhudi ambazo anazifanya Rais sio za kubezwa na
watanzania kwani tunajua kuwa haya ambayo yanafanywa ni manufaa ya wote na sio
ya chama furani jambo la msingi tuzidi kumuombea Rais wetu kwani hata yeye
anasema tumuombe kwa Mungu”Alisema Masele.
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Geita Bw Barnabas Mapande ameitaka migodi
mingine kujitathimini kupitia kampuni ya Barrick na kuwa waaminifu kwenye
kulipa fedha zinazoendana na shughuli wanazozifanya.
Katibu wa CCM wilaya ya Geita Bw Julius Peter amesema hisa ambazo
zimetolewa na Barrick pamoja na Sh Milioni 700 zilizoafikiwa zitasaidia
kuboresha Miundombinu na kuwanufaisha Watanzania wengi
No comments:
Post a Comment