Monday 13 February 2017

WANANCHI MKOANI GEITA KUTOA USHIRIKIANO VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA




Baadhi ya wananchi  mkoani geita  wameahidi kushirikiana na serikali kikamilifu kupiga vita uuzaji  wa dawa za kulevya  kwani zimeleta athari kubwa  kwa vijana pamoja na watoto wadogo katika taifa.
Hatua hiyo imekuja  baada ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda  kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kutoka katika jiji hilo kuanzisha kampeni maalumu ya kutokomeza   uzaji  na usambazaji  wa dawa hizo.

Hali hiyo imepelekea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  kumuapisha Kamishina Rogers Sianga  kwa lengo la kupambana vikali   dhidi ya watu ambao wanaji husisha  na uzaji wa  dawa za kulevya  nchini.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Bwana Selemani Pinde mkaazi wa geita mjini yeye ni mmoja kati ya watu ambao wamepoteza  ndugu zake kutokana na athari za madawa ya kulevya 

Kwa upande wake  Katibu wa vijana wa chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Geita  Bw. Ally Rajabu ameahidi kushirikiana na Serikali kikamilifu kwa lengo la kutokomeza  uuzaji  na usambazaji wa dawa  hizo.


Aidha Diwani wa kata ya Buhalahala   Bw. Mussa  Eliasi amewataka vijana ambao hawana kazi kujiunga katika vikundi mbalimbali ambavyo vinaweza kusababishia kupata mikopo  na kufanya biashara ndogondogo  kuliko kukaa mitaani  jambo ambalo linapelekea  kujiunga katika makundi  mabaya  kama ya utumiaji wa dawa za kulevya.

No comments:

Post a Comment