Wednesday 8 February 2017

MFUMUKO WA BEI TANZANIA WAONGEZEKA KWA KASI KIDOGO



Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) Ephraim Kwesigabo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kuongezeka kwa mfumuko wa bei leo jijini Dar es Salaam. Mfumuko wa bei umeongezeka kutoka asilimia 5.0 kwa mwezi Desemba mwaka jana hadi kufikia asilimia 5.8 mwezi januari 2017.




Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Kijamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) Ephraim Kwesigabo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kuongezeka kwa mfumuko wa bei leo jijini Dar es Salaam. Mfumuko wa bei umeongezeka kutoka asilimia 5.0 kwa mwezi Desemba mwaka jana hadi kufikia asilimia 5.8 mwezi januari 2017.Kulia ni Kaimu Meneja wa Idara ya Takwimu za Ajira na Bei Bibi. Ruth Minja.



Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Kijamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) Ephraim Kwesigabo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuongezeka kwa mfumuko wa bei leo jijini Dar es Salaam. Mfumuko wa bei umeongezeka kutoka asilimia 5.0 kwa mwezi Desemba mwaka jana hadi kufikia asilimia 5.8 mwezi januari 2017.


Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano kuhusu Takwimu za mfumuko wa bei kwa mwezi Januari zilizotolewa na Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Ephraim Kwesigabo (hayupo pichani) leo jijini Dar es Salaam.
Kasi ya mfumuko wa bei za bidhaa na huduma nchini Tanzania umeongezeka kwa kiasi kidogo ukilinganisha na nchi za Afrika Mashariki. 

Takwimu hizo zimetajwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBC), Ephraim Kwesigabo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mfumuko wa bei za bidhaa na huduma kwa mwezi Januari mwaka 2017.

Kwesigabo amesema kuwa nchi zote za Afrika Mashariki hali ya mfumuko wa bei huwa unafanana na kwa kawaida Tanzania inajilinganisha na nchi za awali za Kenya na Uganda kwa sababu nchi zingine zina tofauti kidogo katika utoaji wa takwimu zao.

“Takwimu zilizoishia mwezi Disemba mwaka 2016, zinaonyesha kuwa nchi ya Uganda mfumuko wa bei umeongezeka kutoka asilimia 5.7 hadi asilimia 5.9 na nchini Kenya umeongezeka kutoka 6.35 asilimia  hadi asilimia 6.99 hivyo kwa ujumla mfumuko wa bei Tanzania ni mdogo,”alisema  Kwesigabo.    

Ameongeza kuwa, farihisi za bei zimeongezeka kutoka 100.71 mwezi Januari, 2016 hadi 105.92 mwezi Januari, 2017 wakati mfumuko wa bei za bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi Januari,2017 zimeongezeka hadi asilimia 7.6 kutoka asilimia 7.0 ilivyokuwa mwezi Disemba, 2016.

Kwa takwimu za mwezi kwenye upande wa mfumuko wa bei  za bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula, Mkurugenzi amefafanua kuwa bei za vyakula nyumbani na migahawani zimeongezeka kutoka asilimia 7.4 mwezi Disemba 2016 hadi kufikia asilimia 8.2 kwa mwezi Januari 2017.

Aidha, badiliko la farihisi za bei kwa bidhaa zisizo za vyakula limepungua hadi asilimia 3.6 mwezi Januari,2017 kutoka asilimia 3.8 mwezi Disemba 2016.

Mfumuko wa bei nchini kwa kipimo cha mwaka umeongezeka hadi asilimia 5.2 wakati mfumuko wa bei kwa kipimo cha mwezi Januari, 2017 umeongezeka kwa asilimia 0.8.


No comments:

Post a Comment