Thursday 16 February 2017

MKUU WA MKOA WA GEITA AZUNGUZA NA WANANCHI JUU YA FEDHA ZA TASAF



Mkuu wa mkoa wa Geita, Meja Jenerali mstaafu  Ezekiel Kyunga amefanya ziara ya kutembelea vijiji na mitaa katika wilaya ya Geita lengo likiwa ni kuzungumza na kujua wananchi ambao wanapatiwa fedha  kutoka kwenye mfuko wa kunusuru kaya masikini (TASAF )wanavyofaidika na fedha hizo na namna ambavyo wamezifanyia kazi.
Kyunga ametembelea kwenye kata za  Busanda, Nyakamwaga, Nyanguko, Mtakuja na Bumwangoko na kusitiza wananchi ambao wanapatiwa fedha hizo kutoka kwenye mfuko huo  kutumia kwa maendeleo ambayo yatawasaidia hata baada ya kuwa muda umemalizika wa kupatiwa ruzuku.

Aliongeza kuwa mpango huo sio wa kudumu ni wa miaka mitatu na kwamba hadi sasa wamelipwa awamu kumi  hivyo wamebakiza awamu nane za kulipwa hivyo amewataka kuhakikisha muda uliobaki wanatumia fedha kwa manufaa

Hata hivyo baadhi ya wanufaika wa mradi huo wamesema kuwa tangu kuanzishwa  wamefaidika na vitu vingi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba pamoja na kusomesha watoto hivyo kutokana na hatua hiyo wameishukuru serikali kwa maana imeweza kuwasaidia wale ambao walikuwa awana uwezo.


Pia  katika ziara yake ya siku mbili mkuu wa mkoa wa geita,amekutana na changamoto ya wanufaika wa mradi huo kutokujua kikomo cha  kupokea fedha na wengine kushindwa kutimiza makusudio ya fedha hizo kama ambavyo zimepangwa kufanya shughuli za kimaendeleo na kunusuru kaya ambazo hazina uwezo wa kifedha na kipato na wale ambao walishindwa kuwasomesha watoto


No comments:

Post a Comment