Wednesday 8 February 2017

MARUFUKU UNYWAJI WA POMBE KIHOLELA MJI WA KATORO MKOANI GEITA




Kutokana na kauli ya Raisi wa Jamhuli ya  muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli yakupiga marufu unywaji wa pombe nyakati za asubuhi, hali hiyo imekuwa tofauti katika mamlaka ya mji mdogo wa katoro ambapo kumekuwa  na  baadhi  ya watu ambao wanajihusisha na vitendo hivyo badala ya kutumia  muda huo kuwa  kazini.
Akizungumza mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo wa Katoro Wilayani na Mkoani Geita Bw. Japheti Madoshi amesema kua amepiga marufuku uuzaji wa pombe za kienyeji kiholela pamoja na kuwaomba wananchi kutojihusisha na unywaji wa pombe nyakati za asubuhi na badala yake wajishughulishe katika shughuli mbalimbali kwani bila kufanya hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa mtu atakae  kiuka agizo hili.


Aidha baadhi ya wakazi katika eneo hilo wamepongeza juhudi za serikali ya mamlaka ya mji mdogo wa Katoro kwa kupiga marufu unywaji wa pombe nyakati za asubuhi hali ambayo itapelekea baadhi ya watu wenye tabia  hiyo kuacha mara moja na kujishughulisha katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo .

No comments:

Post a Comment