Monday 9 April 2018

WAKAZI WA CHATO WAMEIPONGEZA SERIKALI KWA KUJENGA SOKO LA SAMAKI




Wakazi wa kata ya Mganza wilayani Chato mkoani Geita wameipongeza Serikali kwa kujenga soko la kimataifa la uzaji wa samaki na dagaa la kasenda kwani limesaidia kuzalisha Ajira mpya kwa baadhi ya wanawake na vijana wilayani humo.

Wakizungumza na mwandishi wetu kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi wa kata hiyo wamesema kuwa kabla ya kujengwa kwa soko hilo hawakuwa na uhakika wakuingiza kipato kwa siku tofauti na sasa ambapo wameanza kunufaika.kupitia ajira za kupakia na kuchambua dagaa.

Diwani wa kata ya mganza Bw.Emanuel Mwita amesema kupitia soko hilo wananchi wake ambao hawakuwa na kazi maalum sasa wamepata kazi   sokoni hapo ambazo zinawaingizia kipato cha kuendesha maisha ya familia zao.

Katika hatua nyingine Bw Mwita ameahidi kuishawishi serikali kuweza kuongeza majengo katika soko hilo yatakayosaidia kuzarisha ajira kwa watu ambao hawajabahatika kupata kazi ya kufanya katika eneo hilo.

No comments:

Post a Comment