Tuesday 24 April 2018

WACHIMBAJI WADOGO GEITA WAPEWA SEMINA YA KUJIKINGA NA MAJANGA WAWAPO KATIKA SHUGHULI ZA UCHIMBAJI

Baadhi ya wachimbaji wadogo wakifuatilia mafunzo ambayo yalikuwa yanatolewa na wakala wa afya na usalama mahari pa kazi na ofisi za Afisa madini Mkoa wa Geita. 

Kaimu meneja wa  wakala wa afya na usalama mahari pa kazi Bw,Mjamo Mohamed akisoma taarifa ya semina hiyo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Kamishina msaidizi wa madini kanda ya ziwa Viktoria Yahaya Samamba akizungumzia juu ya semina hiyo na faida ambazo watazipata wachimbaji kutokana na mafunzo ambayo watapatiwa. 


Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kwaajili ya kuzungumza na wachimbaji wadogo Mkoani Humo wakati wa semina iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Moyo wa Huruma.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Geita ,Leornad Bugomola akielezea tatizo la Kabon kuendelea kusafirishwa kwenda Jijini Mwanza.


Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Gabriel akizungumza na wachimbaji wadogo wa madini Mkoani hapa


Kipindi cha kuanzia Julai 2017 hadi Machi 2018 wachimbaji wadogo Mkoani Geita wameripotiwa kuzalisha kiasi cha Kg. 68.55 zenye Thamani ya TSh. Bilioni 6.5 ongezeko hilo la uzalishaji linatokana na marekebisho ya Sheria ya Madini ya mwaka 2017 pamoja na kanuni zake za mwaka 2018.
Hayo yamebainishwa na mkuu wa mkoa wa Geita mhandisi Robert Gabriel wakati alipokuwa akifungua mafunzo ya siku moja yaliyokuwa yamelenga kuwawezesha wachimbani  wadogo kutambua mbinu za kujikinga na ajali zinazotokana na mvua ambazo zinaendelea Kunyesha.
Mheshiwa Gabriel amesema serikali itaendelea kusimamia na kukusanya mrabaha na tozo kwa kufuata utaratibu wa sheria ambazo zinawataka wachimbaji wadogo kulipa tozo kutokana na shughuli ambazo wanazifanya kwenye maeneo hayo.

Miongoni kati ya mambo ambayo yameonekana ni changamoto ni usafirishaji wa kaboni ya kuchenjuliana madini ya dhahabu kwenda mwanza ambapo  Mkuu huyo amesema wanatarajia kutoa matangazo ya kuzuhia shughuli hiyo ya kusafirisha kaboni na kwamba itatumika ndani ya mkoa huo kutokana na mapato ambayo yameendelea kupotea.

Kamishina msaidizi wa madini kanda ya ziwa Viktoria Yahaya Samamba amesema mapendekezo hayo ni mazuri na kwamba watakaa na wamiliki wa makarasha ili waweze kuwashauri kuwa na mashine ambazo zitasaidia wachimbaji wadogo kutokupeleka kaboni mwanza na shughuli hizo zitakuwa zikifanyika Mkoani humo.

Aidha kwa upande wake  kaimu meneja wa  wakala wa afya na usalama mahari pa kazi Bw. Mjamo Mohamed  alisema kuwa wameamua kukaa na wachimbaji kutoa semina ya kujikinga na majanga kwenye maeneo yao ya kazi kutokana na mvua ambazo zimeendelea kunyesha hivyo kufanya hivyo kutawasaidia kuepukana na majanga ambayo yanaweza kusababisha watu kupoteza Maisha.


Hata kwa kwa upande wa mmoja kati ya wachimbaji wadogo ambaye amezungumza na mtandao huu, ameishukuru ofisi ya madini mkoani humo pamoja na wakala wa afya na usalama mahari pa kazi kuendesha semina hiyo na kwamba imewajenga na pia imewapa mwangaza kwani wametambua namna ambavyo wanaweza kujikinga na majanga kwenye maeneo yao ya kazi ikiwa ni pamoja na kuwapima afya watu ambao wanawaajili kwenye shughuli zao.

No comments:

Post a Comment