Sunday 8 April 2018

GEITA YAKABIDHI MWENGE WA UHURU MKOANI KAGERA


Mkuu wa Geita,Mhandisi Robert Gabriel akimkabidhi mwenge wa uhuru Mkuu wa mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu mapema leo.


Mkuu wa mkoa wa Kagera  Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu akipokea Mwenge wa uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Gabriel mapema leo.




Kamanda wa Polisi Mkoani Geita,Mponjoli Mwabulambo akiruka pamoja na vijana wa kikosi cha kutuliza ghasia na baadhi ya wakuu wa idara mbali mbali kutoka kwenye halmashauri za wilaya




Mkuu wa mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Gabriel akiwapongeza wananchi pamoja na wakuu wa idara ambao wameshiriki kwenye zoezi la ukimbizaji wa Mwenge uhuru.


Mkuu wa mkoa wa Kagera ,Meja jenerali Mstaafu,Salum Kijuu akisoma taarifa ya miradi ambayo itapitiwa na mwenge wa uhuru.
Mwenge  wa uhuru umeliza mbio zake Mkoani Geita na kukabidhiwa mkoa wa  Kagera huku miradi mitano ikishindwa kuzinduliwa kutokana na taarifa ya gharama za miradi hiyo kutofautiana na ya Mkoa.

Akisoma taarifa ya shughuli za mbio za mwenge wa uhuru zilivyofanyika Mkoani Humo,Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel  amesema  jumla ya miradi sitini na tatu yenye thamini ya sh ,bilioni 12.7  imepitiwa na mwenge wa uhuru  huku mitano ikishindwa kuzinduliwa  serikali ikiendelea na  uchunguzi kubaini tatizo la miradi ambayo haikuzinduliwa  na kwamba tayari TAKUKURU wamekiwisha kuagizwa kufanya uchunguzi wa kina kwenye miradi hiyo.

Sanjali na hayo Mhandisi Robert Gabriel ameelezea mmomonyoko wa maadili  ambavyo umeendelea kulikumba Taifa na kwamba kupitia mbio hizo awana budu kuendelea kukemea na kulaani vitendo hivyo ambavyo vimekuwa vikiwaelemea zaidi  vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa.

Aidha Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru  Kitaifa ,Charles Kabeho amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Geita kwa namna ambavyo wameweza kutumia fedha za lipa kutokana na matokeo sasa  kwa kujenga majengo mazuri ya madarasa kwa Bei nafuu Zaidi.
 Mkuu wa mkoa wa Kagera Meja jenerali mstaafu Salum Kijuu amesema  miradi ambayo itapitiwa na mwenge wa uhuru  ni 80 na thamani yake ni bilioni 11 na halmashauri nane ndizo ambazo zitapitiwa.

Mwenge wa uhuru umeanza mbio zake leo Mkoani Kagera ambapo  utakimbizwa  kwenye halmashauri nane  huku kauli mbiu ikiwa ni elimu ni ufunguo wa maisha wekeza sasa kwa maendeleo ya Taifa letu.

No comments:

Post a Comment