Wednesday 18 April 2018

NAIBU MASAUNI AWATAKA WANANCHI KUWEKA FEDHA BENKI, AZIOMBA TAASISI ZA KIFEDHA ZA KIISLAMU AFRIKA KUONGEZA KASI KUWEKEZA NCHINI


 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza katika Mkutano wa Tano wa Taasisi za Fedha za Kiislamu Afrika uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam. Masauni aliwataka Watanzania kuweka Fedha zao katika Benki za Kiislamu zilizopo nchini ambazo hazina riba ili ziwasaidie katika mafanikio mbalimbali. Pia Masauni aliipongeza Taasisi hiyo kwa kuwekeza nchini. Kulia ni Kamishna wa Bima katika Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima nchini (TIRA), Dk. Baghayo Saqware, na katikati ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Bernard Kibesse. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi za Fedha za Kiislamu Afrika, Muhammad Mughal alipokua anaishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano wake kwa Taasisi yake. Hayo alizungumza katika Mkutano wa Tano wa Taasisi hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam. Masauni aliwataka Watanzania kuweka Fedha zao katika Benki za Kiislamu zilizopo nchini ambazo hazina riba ili ziwasaidie kupata mafanikio zaidi. Wapili kulia ni Kamishna wa Bima katika Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima nchini (TIRA), Dk. Baghayo Saqware, na watatu kulia ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Bernard Kibesse. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza katika Mkutano wa Tano wa Taasisi za Fedha za Kiislamu Afrika uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam. Masauni aliwataka Watanzania kuweka Fedha zao katika Benki za Kiislamu zilizopo nchini ambazo hazina riba ili ziwasaidie katika mafanikio mbalimbali. Pia Masauni aliipongeza Taasisi hiyo kwa kuwekeza nchini. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati), akimpa zawadi Kamishna wa Bima katika Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima nchini (TIRA), Dk. Baghayo Saqware. Kushoto ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Bernard Kibesse, kulia ni Balozi wa Nigeria, nchini, Dk. Sahab Isa Ga, na wapili kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi za Fedha za Kiislamu Afrika, Muhammad Mughal. Mkutano wa Tano wa Taasisi hiyo umefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo Masauni alikua mgeni rasmi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 




Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wanne kutoka kulia mstari wa mbele), akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Taasisi za Fedha za Kiislamu Afrika pamoja na washiriki wa Mkutano wa Tano wa Taasisi hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam. Masauni ambaye alikua mgeni rasmi katika mkutano huo, aliwataka Watanzania kuweka Fedha zao katika Benki za Kiislamu zilizopo nchini ambazo hazina riba ili ziwasaidie kupata mafanikio zaidi. Pia Masauni aliipongeza Taasisi hiyo kwa kuwekeza nchini. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment