Tuesday 3 April 2018

MATUKIO MBALIMBALI YALIYOJIRI BUNGENI LEO APRIL 04, 2018



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akiteta jambo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakati wa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kumi na Moja wa Bunge la Tanzania, Leo Mjini Dodoma.




Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akijibu hoja za wabunge wakati wa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kumi na Moja wa Bunge la Tanzania, Leo Mjini Dodoma.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akiwasilisha Bungeni azimio la Bunge la Kuridhia makubaliano ya Paris chini ya mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu mkataba wa mabadiliko ya Tabia nchi, Leo Mjini Dodoma.





Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mh. Jenista Mhagama akiteta jambo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk Adelardus Kilangi, wakati wa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kumi na Moja wa Bunge la Tanzania, Leo Mjini Dodoma.

No comments:

Post a Comment