Tuesday 3 May 2016

WAFANYABIASHARA WA SUKARI MKOANI GEITA WAIOMBA SERIKALI KUPUNGUZA BEI PINDI SUKARI KUTOKA NJE ITAKAPOANZA KUINGIA NCHINI

 
Wafanyabiashara wa sukari mkoani Geita wameiomba serikali pindi itakapoanza zoezi la kuongeza sukari kutoka katika viwanda vya nje ya nchi kupunguza gharama za manunuzi ya bidhaa hiyo ili waweze kuuza kwa shilingi 1800 kwa kilo kama bei elekezi tofauti na ilivyo sasa.

Hayo yamesemwa na wafanyabiashara kwa nyakati tofauti walipokuwa wakizungumza na storm habari mapema hii leo mkoani hapa.

Akizungumza kwa njia ya simu kaimu afisa biashara wa halmashauri ya mji wa Geita bw, George Mpogomi, amesema kuwa upangaji wa bei ya sukari unategemea gharama za ununuaji wa bidhaa yenyewe kutoka katika sehemu husika.

Awali waziri mkuu wa Tanzania mh, Kassim Majaliwa akiwa katika bunge la 11 alitangaza kuagiza sukari kiasi kutoka katika viwanda vya nje ili kupunguza adha ya kupanda kwa bei ya sukari nchini huku akiwataka wafanyabiashara kuacha kupandisha bei ya sukari kiholela bila ya kufuata utaratibu.


No comments:

Post a Comment