Tuesday 17 May 2016

BAADHI WAFANYABIASHARA WA SOKO KUU JIJINI MWANZA WAANDAMANA NA KWENDA KWA MKUU WA WILAYA YA NYAMAGANA







Wafanyabiashara  wa  Soko Kuu  jijini  Mwanza wameandamana kwenda kwa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana ni baada ya kikao chao na Mkurugenzi wa jiji kutokufikia muafaka.
Akizungumza na  Storm habari  Mwenyekiti wa Soko hilo Bw.Khamadi Nchola  amesema kuwa kikao  cha  kutazama  tenda upya kimeshindikana  kufikia muafaka baada ya ofisi ya Mkurugenzi  kubaki na msimamo  wa  awali wa kupandisha kodi.

Awali  wafayabiashara wenye   meza  na migahawa walilipa sh. elfu 10,000/=  na sasa ni   sh.elfu 50,000/=  huku wa vyumba vya maduka na vioski  sh.elfu  20,000/= sasa ni sh. laki 100,000/=kitendo amabacho wamekiita kuwa ni unyanyasaji na kwamba wamelipeleka  mbele ili lishughulikiwe zaidi  kabla  ya hatua nyingine.

Aidha Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza Bw.Adam Mgoyi aliitisha kikao na kuketi na wafanya bishara  hao baada ya kutishia kugoma kutokana na mabadiliko ya malipo ya tozo za pango na kuongezeka  karibu  mara nne sasa.


No comments:

Post a Comment