Tuesday 17 May 2016

AFISA ARDHI WA HALMASHAURI YA MJI WA GEITA BW.MABULA GOGODI AINGIA KWENYE MGOGORO NA WANANCHI WA MTAA WA MWATULOLE MKOANI GEITA



Wananchi wa mtaa wa Mwatulole mkoani Geita wamemtaka  Afisa  ardhi  wa Halmashauri ya mji wa Geita Bw.Mabula Gogodi  kuwapatia  maelezo ya kina kuhusu kupima ramani za Barabara za mtaa huo bila kuwashirikisha hali ambayo imepelekea huduma za kijamii  kusuasua.

Afisa huyo, amejikuta akiwa katika wakati mgumu mbele ya mwenyekiti  mtaa huo, Charles Fikiri, ambapo sauti yao ilikuwa ni moja tu ni kwanini apime viwanja na kuzigeuza baadhi ya barabara kuwa viwanja vya kujenga  makazi  ya  watu.

Afisa huyo amegoma kuzungumza na  storm habari kwa kigezo kuwa yeye si msemji, lakini kinasa sauti iliweza  kunasa mazungumzo yake wakati akiwafafanulia wananchi baadhi   ya  mambo.

Aidha kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa Mwatulole Charles Fikiri,amesema kuwa wakati wa ramani zinapochorwa mara nyingi mipango miji wamekuwa hawashirikishi jamii na mwisho wa siku matatizo kama hayo hujitokeza mara kwa  mara.


Hadi storm habari inaondoka katika eneo la tukio imeshuhudia  wananchi wakiondoa vigingi vya mawe katika eneo ambalo linasadikika ndipo ilipokuwa barabara na kugeuzwa uwanja  wa  makazi.

No comments:

Post a Comment