Sunday 1 May 2016

SHEREHE ZA MEI MOSI: RAIS MAGUFULI ASEMA WAFANYAKAZI HEWA WAMEFIKIA 10,295

Idadi wa watumishi hewa nchini  imeendelea kuongezeka ambapo takwimu za jana zinaonyesha kuwepo kwa watumishi hewa 10,295

Akizungumza  leo wakati wa maadhimisho ya sherehe za Mei Mosi,  Rais  wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania  Dr John Pombe Magufuli amesema kati ya watumishi hao hewa, 8,373  wanatoka  Tamisemi   na watumishi 1.922 wanatoka serikali kuu.

Amesema watumishi hao walikuwa wakiligharimu taifa sh. Bilioni 11.6 kwa mwezi sawa na Bilioni 139  kwa  mwaka.

No comments:

Post a Comment