Tuesday 13 September 2016

MGODI WA DHAHABU WA GEITA(GGM) WASAIDIA KUTATUA TATIZO LA WATU KUPOTEZA MAISHA KUTOKANA NA KUNUSA SUMU YA SAYONAIDI ( CYONIDE ) MKOANI GEITA



Kutokana na Madhara ambayo  yamejitokeza katika  Kijiji  na Kata  ya Busanda kusambaa kwa Sumu   ya Sayanaidi, Mgodi wa Dhahabu  wa Geita(GGM) imeguswa na tukio hilo na imetuma wataalam kwa ajili ya  kutatua  tatizo  ambalo wananchi wameendelea kuathirika   kutokana  na baadhi   yao kulamba  na kunusa  Sumu  hiyo.

Meneja Mahusiano ya Jamii wa Mgodi huo Bw.Manase Ndoroma amesema kuwa wao kama Mgodi wamesikia  Janga hilo na kwasababu wao wana uwezo   wa  kutatua   Janga hilo ndio maana wameguswa na kuamua kutoa msaada kwa  watu  ambao wamekwisha athirika na baada ya kusikia kwamba kuna kifo cha mtoto  wa miaka minne ambaye alilamba  sumu  hiyo  na kupoteza   maisha.

Baadhi ya Wananchi ambao wamedhurika na Sumu hiyo Bi.Maria Kaziza na Bw.Kaverwa   Lubuga, wamesema kuwa  wameathirika kutokana na kwamba mifugo mingi imepoteza maisha pamoja na wao kwa sasa hali  za afya wanajisikia sio nzuri kwani makoo yamekuwa yakikauka kutokana na kutumia Sumu hiyo.

Hata hivyo Diwani wa kata hiyo Elias  Kisome amelaani   kitendo  cha wamiliki wa machimbo madogo kusafirisha Sumu  kwa  njia  ya Pikipiki na badala  yake  kutumia vyombo  ambavyo  ni  vya uhakika vya kusafirishia Sumu.


Akizungumza kwa njia ya simu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mponjoli Mwabulambo amesema yuko nje ya Mkoa na Habari hizo amezisikia  na uchunguzi    unaendelea ili kubaini chanzo cha Sumu hiyo.

No comments:

Post a Comment