Baadhi ya Wafanyakazi na Watangazaji wa Stormfm wakibadilishana mawazo siku ya Jana katika Ukumbi wa Desire Park
Wakiwa katika picha ya pamoja Baadhi ya Wafanyakazi na Watangazaji wa Stormfm
Watangazaji wa Kipindi cha Storm Asubuhi katika picha ya pamoja, kulia ni Helena Maduhu, kati ni Joel E.Maduka na kushoto ni Paul Williams.
Watangazaji wa Kipindi cha Kijiweni wakiwa na Dj, Kulia ni Orest Ngowi,kati ni Ester Mabula na Kushoto Ni Deejay Kg
Tukio la kukata keki lilianza lakini picha kwanza kabla ya kukata
Muda wa Maakuli na Pichani ni Mkurugenzi wa Vipindi(PM) Chris Lugoe akipata chake
Kijiweni Masters Orest Ngowi na Ester Mabula
Kwanza Shukrani za Dhati kwa Mwenyezi Mungu kwa upendeleo wake kwetu sote
kwa kutubariki na kutupatia pumzi ambayo tunatumia bila gharama yoyote ,Tunachukua
nafasi hii kukushukuru sana wewe msikilizaji pamoja na mtembeleaji wa mitandao yetu ya Kijamii ikiwa Instagram,Facebook,Twitter,Tovuti pamoja na Blog yetu ambae umeendelea kutufatilia kwa
vipindi mbali mbali vinavyorushwa na kituo chako bora cha matangazo kanda ya
ziwa Ukuwa ndani na nje ya mkoa wa Geita.
Storm fm ni Kituo cha radio kilichopo Mkoani Geita,ambacho kinasikika
kanda ya ziwa na kwa njia ya mitandao kama Tovuti yetu ambayo ni Stormfm.co.tz
pamoja na Tunein, Ni kituo cha Biashara kilichoanzishwa tarehe 18 September
2014 na leo hii kinatimiza miaka Miwili
Tangu kuanza Shughuli za Utangazaji
Kimeendelea kuwa Mkombozi Mkubwa kwa Kuhabarisha,Kuelimisha,Kuasa na Kuburudisha
kupitia vipindi mbali mbali ambavyo vimekuwa vikifanyika kituoni hapo.
Ahadi ambayo timu nzima ya Stormfm inatoa kwako ni Kutanua wigo mkubwa wa
matangazo ili kufikia idadi kubwa ya Watanzania pamoja na kutoa habari na
taarifa zenye Uhakiki na Sahihi kwako.
Miaka Miwili Kwenye Kasi tunasema Spidi Bado Ni Ileile.
Asante Kwa Ushirikiano Wako.
No comments:
Post a Comment