Monday 26 September 2016

AFISA UVUVI NA MRATIBU ELIMU WAWEKWA CHINI YA ULINZI KWA MADAI YA KUTETEA UVUVI HARAMU

Afisa Uvuvi kata ya Nkome Merina Damian na Mratibu Elimu Kata Thom Sharusanga wamewekwa chini ya ulinzi na Mkuu wa Wilaya ya Geita Herman Kapufi baada ya kudaiwa kuhusika kuwatetea wavuvi haramu ambao wamekuwa wakijihusisha kuvua samaki ambao hawaruhusiwa kwa kutumia nyavu haramu za dududuu.

Hatua ya kusimamishwa imekuja baada ya Mwenyekiti wa kitongoji Simon Kinasa kuanzisha operesheni na kuwakamata baadhi ya watu wanaovua samaki chini ya kiwango ambapo baada ya kuwakamata afisa uvuvi na Mratibu wakamuamuru awaachie wakidai mwenyekiti amewakamata kwa madai amenyimwa rushwa.

No comments:

Post a Comment